Baa-Medi

Usiku mnene

Mwenyewe kwenye kichochoro

Tochi haina mawe- giza totoro

Mvua,Radi hadi malinzi washadoro

Hatari Mbwa Wakali Wamekata Minyororo

 

Chocho Ngalimi -Si chocho Ngarenaro

Utamwambia nini– sahiyo kumi kasoro

hutoka Kazini -na mfuko wa malboro

Hatari Mbwa wakali wamekata Minyororo

 

mezani Makombo-hukombeleza kama soro

mabaki ya nyama choma na makongoro

silaha ya baamedi kwenye vichochoro

hatari Mbwa wakali wamekata minyororo

 

we chukulia mzaha- amenizaa ni mzazi

kazini ni baa - we huenda baada ya kazi,

weekend balaa – ye hutingwa na kazi

Njaa-Hatari mbwa wakali wamekata minyororo

 

Usiku mmoja hupiga kazi ka msukule

mi humngoja- nimsimulie za shule

Hurudi mchovu na asiyetaka kelele

Shukrani-Mkono kinywani Daily

 

Usingizi baada ya simulizi ni njozi

Njozi ya ufumbuzi Utatu Utatuzi

Kazi ni Kazi- Kazini kwake ni Baa

Namuita Mama we muite Baamedi

-Matei Babu 2016

This poem is about: 
My family

Comments

Additional Resources

Get AI Feedback on your poem

Interested in feedback on your poem? Try our AI Feedback tool.
 

 

If You Need Support

If you ever need help or support, we trust CrisisTextline.org for people dealing with depression. Text HOME to 741741